Vifo Ajali ya Lori la Mafuta Morogoro Vyafika 101


Idadi ya vifo vya majeruhi wa ajali ya lori la mafuta iliyotokea mkoani Morogoro, imefika 101 baada ya majeruhi mmoja aliyekuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kufariki dunia usiku wa kuamkia jana.

Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano MNH, Aminiel Aligaesha, alisema aliyefariki dunia ni Sadiki ismail (31).

Alisema mpaka sasa kati ya majeruhi 47 waliofikishwa hospitalini hapo, waliobaki ni 14 ambapo kati yao 11 wako katika Vyumba vya Uangalizi Maalum (ICU) na watatu wako katika wodi za kawaida na hali zao zinaendelea vizuri.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad