Walimu Wapigwa STOP Kuingia na Viboko Darasani

Walimu  wa madarasa ya awali hadi la tatu kote nchini,  wamepigwa marufuku kuingia darasani na viboko kwa kuwa kufanya hivyo ni kuongeza woga  kwa wanafunzi na kusababisha utoro.

Mkurugenzi Msaidizi Elimu ya  Msingi kutoka Ofisi ya Raisi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Jidamva, alisema hayo akiwa kwenye ziara ya siku moja  mkoani Kilimanjaro.

Alisema licha ya sheria kuruhusu wanafunzi kuchapwa voboko, utafiti unaonyesha  kuwa  mwalimu anapoingia  darasani na kiboko, humtia mwanafunzi uoga na kusababishia wanafunzi wengi wa  madarasa ya awali hadi la tatu kuchukia shule na kuacha.

"Watoto hao ni wadogo na  wana uwezo wa kuonyeka bila kutumia fimbo. Naagiza  walimu wote kuacha kutumia fimbo wanapoingia madarasani na badala yake kuwatengenezea wanafunzi mazingira rafiki ili kuwawezesha kuipenda elimu na kufanya   vizuri katika masomo yao,” alisema.

 Alisema mbali na kutoingia  na viboko madarasani, pia  walimu wakuu  katika shule za msingi kuhakikisha madarasa ya awali  hadi la  saba yanaongea vyema ili kuleta mabadilikio ya kimaarifa kwa wanafunzi nchini.

"Tumepata mradi  katika mikoa ya Mwanza na Kilimanjaro, ambapo  ulituwezesha kuwasaidia wanafunzi wa madarasa ya awali lakini mradi huo kwa sasa umeondoka na katika ziara yangu ya siku moja mkoani Kilimanjaro naona  walimu  wameweza kuuendeleza licha ya mradi huo kumaliza muda wake" alisema.

"Madarasa ya awali yanaongea, sasa nataka maofisa elimu mkoa wa Mwanza na Kilimanjaro hakikisheni mnakuwa walimu kwa mikoa mingine ambayo haikupata mradi huu ili kuhakikisha  Tanzania nzima madarasa ya awali hadi la tatu yanaongea kupitia rasilimali zinazotuzunguka."

Katika ziara hiyo, Jidamva alitembelea  shule za msingi za Kifumbu na Rau kuona juhudi za uboreshaji wa  madarasa ya awali kabla ya kusambazwa nchini kote.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad