Chris Brown kuwa ‘Bestman’ harusi ya Davido


Msanii wa muziki kutoka nchini Nigeria, Davido Adedeji Adeleke maarufu kama Davido amefunguka juu ya msanii nyota kutoka Marekani, Chris Brown kumsimamia kwenye harusi yake anayotarajia kufunga na mchumba wake Chioma ambaye siku chache zilizopita alimvalisha pete akiwa mwenye ujauzito wake.

Davido kupitia ukurasa wake wa Tweeter amesema kuwa msanii huyo nyota kutoka Marekani atakuwa mpambe wake (Best man) siku yake ya harusi ambayo anatarajia kufanya mwaka 2020.

“Chris amesema anataka kuwa mpambe wangu, hebu fikiria unamuona Chris kwenye vazi maalum la heshima, Chris amekubali kuwa mpambe wangu hebu vuta picha Chris yuko pembeni yangu” amesema Davido.

Mbosso afichua siri yake na marehemu Boss Martha
Aidha, Chris Brown amekuwa shabiki mkubwa sana wa nyimbo za Davido na mara kadhaa kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii amekuwa akijirekodi akisiiliza baadhi ya ngoma za Davido.

Hatua hiyo ilipelekea wawili hao kufanya ngoma ya pamoja inayoitwa ‘Blow mind’ ambayo ni moja ya ngoma nzuri kuwahi kufanyika kutoka kwa wasanii wakubwa Afrika na Ulaya.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad