Membe: Bila uhuru wa vyombo vya habari, serikali itakuwa dumavu



Mwili wa mwili wa mwandishi wa habari nchini Tanzania, Godfrey Dilunga (43) umeagwa leo Alhamisi katika viwanja vya Mnazi mmoja, Dar es Salaam kisha utasafirishwa kwenda mkoani Morogoro kwa mazishi yatakayofanyika kesho Ijumaa.

Dar es salaam. Aliyekuwa waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania, Bernard Membe amesema Serikali inaweza kuwa  dumavu endapo haitaruhusu uhuru wa vyombo vya habari Tanzania.

Membe ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Septemba 19, 2019 wakati shughuli ya kuaga mwili wa mwandishi wa habari nchini Tanzania, Godfrey Dilunga (43) katika viwanja vya Mnazi mmoja, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wanahabari, viongozi wa serikali, pamoja na wanasiasa mbalimbali.

Dilunga aliyefariki dunia Septemba 17, 2019 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dar es Salaam alipokuwa amelazwa kwa matibabu ya homa ya tumbo.

Akitoa salamu zake za rambirambi mbele ya wanahabari hao, Membe amesema Dilunga ameondoka akiwa anastahili heshima ya Taifa kupitia kazi yake ya uandishi wa habari.

"Siku hii tunapomuaga Dilunga, itukumbushe uhuru wa vyombo vya habari, kazi ya uandishi wa habari ni sawa na mbolea, unapoiweka katika mche inachipua."

"Bila kazi ya vyombo vya habari, serikali itakuwa dumavu, vyama vya siasa havitakuwa na afya," amesema Membe
Tags

Post a Comment

4 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Sasa mkia umeshatibiwa....¿!!!???
    B. kameliosi .upo ndugu yangu..Konki..

    Hivyo ni wa Jimbo gani pesa zetu za Libya uzilete katika Miradi yya Maendeleo chonde chonde cha halamu hakiliki huwa kinatokeaga PUANI.

    Usingoje hivyo. fanya kama wale kna nani Waliorudishaga.
    Siio Aibu ila ni UZALENDO NA KUKOMAA.

    TUNANGOJA KABLA YA KUKUFATA SI UNAJUA DIWANI ANA KOFIA MBILI NA NI MUADILIFU

    ReplyDelete
    Replies
    1. Swadakta, JPM Ameichunia anaangalia Mchongo na Mlolongo wote. Akilivalia njuga Mtacheza SINDIMBA. Kwachu kwachu.

      Delete
  2. Sasa mkia umeshatibiwa....¿!!!???
    B. kameliosi .upo ndugu yangu..Konki..

    Hivyo ni wa Jimbo gani pesa zetu za Libya uzilete katika Miradi yya Maendeleo chonde chonde cha halamu hakiliki huwa kinatokeaga PUANI.

    Usingoje hivyo. fanya kama wale kna nani Waliorudishaga.
    Siio Aibu ila ni UZALENDO NA KUKOMAA.

    TUNANGOJA KABLA YA KUKUFATA SI UNAJUA DIWANI ANA KOFIA MBILI NA NI MUADILIFU

    ReplyDelete
    Replies
    1. Tena hili Movie linatisha.
      Patamu hapo.

      Walio katika Mikia itabidi wafunge BENDEJI. Manake POP siyo saizi yao.

      Delete

Top Post Ad

Below Post Ad