Meya Atoa Muafaka Wauza Mihogo Coco Beach


Meya wa Manispaa ya Kinondoni Benjamini Sitta, ametoa mwezi mmoja na nusu kwa wafanyabiashara wa Mihogo katika ufukwe wa Coco, wawe wamehama na kupisha zoezi la ujenzi wa ufukwe huo unaotarajiwa kuanza Novemba 5, 2019.


Akizungumza na wafanyabiashara hao leo Septemba 18, Meya Sitta amewapa eneo jingine litakalokuwa karibu na sehemu yao ya awali na rahisi kufikiwa na wateja wao wa awali.

''Novemba 5, 2019 tunapiga bati, tunaamini kipindi hiki, eneo mtakuwa mmeshaliona na nyinyi taratibu mtaanza kwenda na muwasaidie akina Mama wajane wapate sehemu nzuri, hao wateja wanaokuja hapa kufika pale itakuwa ni rahisi, mkiamua kwenda pale kwenye kituo cha Polisi hadi kwenye maua kule ni sawa'' amesema Meya.

Hatua hii imekuja ikiwa ni siku chache tu tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, alipoagiza watendaji katika Jiji la Dar es Salaam kuhakikisha wanaisimamiwa vyema miradi ambayo imekuwa ikisuasua
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad