Mo Dewji aibua mjadala mtandaoni, aomba radhi


Dar es Salaam. Mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania, Mohamed Dewji ‘Mo’ ameibua mjadala mtandaoni baada ya kuweka ujumbe uliowaibua wachangiaji kumbushia tukio la kutekwa kwake.

Mo ambaye ni mwekezaji wa Klabu ya Simba jana Jumanne Septemba 17, 2019 aliweka ujumbe kwenye akaunti yake ya Twitter akisema, “Kuna maisha ya mtandaoni na maisha halisi.”

Ujumbe huo umejadiliwa kwa mitizamo tofauti huku wengine wakikumbushia bilionea huyo namba moja kijana Barani Afrika alivyotekwa na watu wasiojulikana jinsi watu walivyotumia mitandao hiyo kupaza sauti zao.

SOMA ZAIDI: Ujumbe wa Mo Dewji wagusa wengi mtandaoni

Alfajiri ya Oktoba 11 mwaka 2018, Mo alitekwa na watu wasiojulikana maeneo ya hoteli ya Collessium jijini Dar es Salaam alikokwenda kwa ajili ya mazoezi.

Tukio la kutekwa kwake lilitikisa ndani na nje ya nchi na mitandao mbalimbali ilijadili suala hilo la kutekwa kwake hadi Oktoba 20, 2019 watekaji walipomtelekeza akiwa hai katika viwanja vya Gymkhana Dar es Salaam.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad