Mtalii Aliyefariki kwa kuzama baharini akiwa anamchumbia mpenzi wake, mwili wake wachukuliwa na Ubalozi wa Marekani

Mwili wa Mtalii raia wa Marekani, Steven Weber, aliyefariki kwa kuzama baharini akiwa anamchumbia mpenzi wake, Kenesha Antoine umechukuliwa na ubalozi wa Marekani kwa ajili ya uchunguzi wa kina na taratibu za mazishi.

Katibu mtendaji kamisheni ya utalii visiwani Zanzibar, Abdalla Mohamed amesema taarifa kutoka kituo cha Konde, Pemba zinaeleza kuwa mtalii huyo alifariki akiwa anaogelea baharini.

Moja ya video iliwaonesha Weber na Kenesha wakiwa katika mazingira ya hoteli walichopanga na chumba hicho kilichozungukwa na vioo kimejengwa chini ya maji katika hoteli moja kisiwani Pemba.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad