Web

Tundu Lissu Abadili Tarehe ya Kurudi Tanzania


Mwanasiasa wa upinzani nchini Tanzania, Tundu Lissu, amebadili tarehe yake ya kuja nchini baada ya kuarifiwa kuwa daktari wake kusema anataka kumuona Oktoba 1 mwaka huu.

Kipindi cha nyuma Lissu alidokeza kuwa atarudi Septemba 7 ambayo itakuwa ni Jumamosi ya wiki hii, hata hivyo Lissu sasa anasema bado anasubiri kupata ridhaa ya madaktari wake iwapo anaweza kurudi nyumbani.

"Nilisema mwanzoni kwamba nitarudi tarehe 7 septemba ya mwaka huu ambayo ni Jumamosi ya keshokutwa lakini mpaka sasa hivi sijapata ruhusa ya madaktari wangu, dakari wangu ameniambia ataniona tarehe 1 Oktoba na kwa mara ya mwisho ataniona tarehe 8 Oktoba," amesema Lissu.

"Kwahiyo hii tarehe ya mwisho ya 7 Oktoba haitawezekena kwasababu daktari wangu anahitaji kuniona kwenye hizo tarehe 2 baada ya hapo ntafanya utaratibu wa kurudi nyumbani."

 Septemba 7 ni miaka miwili tangu Lissu kushambuliwa na watu wasiojulikana huko Jijini Dodoma.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad