VIDEO: Rose Muhando Aibuka Kwa Kumsifia Kenyatta


Muimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania, Rose Muhando ametoa shukrani kwa Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta na wananchi wake kwa kumsaidia kipindi alipokuwa na matatizo ya afya.

Ambapo mwaka jana kulisambaa baadhi ya video zikimuonesha akiwa katika moja ya kanisa akifanyiwa maombi ya kutolewa mapepo Jijini Nairobi kwa kudaiwa kutumia madawa ya kulevya yaliyomdhoofisha.

Shukrani hizo amezitoa kupitia wimbo wake mpya aliouachia Jumanne, Septemba 24 akiwashukuru juu ya uponyaji uliofanyika pindi akiwa katika ardhi hiyo ya Kenya.

“Shukrani zangu kwa taifa viongozi na wananchi wa Kenya kwa kuokoa maisha yangu, mlifungua milango yenu na kunikaribisha kwa mikono yenu miwili. Kwa hakika Kenya ilinionesha neema. Sijui jinsi ambavyo ninaweza kuwalipa kwa upendo wenu kwa kuwa mimi si tajiri lakini naomba Mungu aibariki Kenya”, ni sehemu ya maneno yaliyopo katika wimbo huo wa Rose Muhando.

VIDEO:
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad