Ed Sheeran Atajwa kama Mwanamuziki Mwenye Thamani zaidi Uingereza


Msanii wa muziki kutoka nchini Uingereza, Ed Sheeran ametajwa kuwa ndiye mwanamuziki tajiri zaidi kwenye kundi la watu maarufu wenye umri chini ya miaka 30 nchini humo akiwa na thamani ya paundi milioni 170.

Kuongezeka kwa thamani ya Ed kumejiri mara mbili ndani ya kipindi cha miezi 12 na ndiyo sababu iliyomfanya kumnyang’anya nafasi ya kwanza mwanamuziki Adele.

Katika orodha hiyo sasa nafasi ya pili imechukuliwa na muigizaji wa filamu maarufu ya ‘Harry Potter’ Daniel Radcliffe akiwa na thamani ya paundi milioni 90 huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na Harry Styles kutoka kwenye kundi la zamani la One Direction, akiwa na paundi takribani milioni 64.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad