Jamaa Apima DNA Watoto Wake 3, Agundua Wawili Sio Wake.....

Jamaa huyu wa Nigeria kwa jina la Ijimakiwa Dayo ameibukia Facebook kueleza kuwa anajuta kuoa mwanamke huyo kwa miaka 12 kwani amegundua kuuziwa mbuzi kwenye gunia ambapo kati ya watoto watatu waliozaliwa ndani ya ndoa yao wawili sio wake wa kwanza akiwa na miaka 11 sasa

Amesema hivi karibuni mkewe alibadilika sana, Pia akawa anamuibia pesa mara Kwa Mara Mara ikiwemo kumuibia naira million 1 ya Nigeria takribani millioni 6.3 za Kibongo. Alimfungulia pia duka mke huyo lakini akawa haachi wizi wa pesa zake. Ambapo mara Kwa Mara alikuwa akitoka na watoto hao watatu. Ikatokea jamaa akawauliza watoto hao huwa mnaenda wapi na mama yenu wakamwambia kwa anko flani ndipo kengele ya tahadhari ikamjia akaanza uchunguzi Kwenye akaunti ya Facebook ya mkewe huyo ambapo mmoja wa ex wa mkewe alionekana kufanana na mtoto wa kwanza

Baada ya kwenda kupima DNA majibu yameonesha licha ya watoto wote kuzaliwa ndani ya ndoa yao lakini mtoto wa kwanza na wa Mwisho ambao wote ni wa kiume sio wake bali mtoto wa pili ambaye ni wa kike ndie wake. Lakini amesema hata alipomuuliza mkewe huyo hakuonekana kushtuka wala kujali kuonesha kuwa anaujua mchezo wake muda mrefu

Kwasasa mke huyo ametokomea kusikojulikana na watoto hao ambapo jamaa kupitia Facebook ametaka wanaojua alipo wamuibue akionekana kuwa na hasira sana
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad