Kitenge: "Nimetua Rasmi Wasafi FM" Lulu Michael Awa Mbadala Wake EFM


MTANGAZAJI maarufu wa Habari za Michezo Tanzania, Maulid Kitenge ‘chumvi’ ameweka wazi kuwa ameachana na Kituo cha Redio cha EFM na kujiunga Wasafi  FM inayomilikiwa na mwanamuziki, Diamond Platinumz.


Maulid Kitenge alikuwa mtangazaji wa EFM tangu mwaka 2015 akiwa kama Mkuu wa Idara ya Vipindi vya Michezo, huku akitangaza vipindi vya michezo vya Sports Headquarters na E-Sport, pamoja na kusoma magazeti kwenye Kipindi cha Joto la Asubuhi ndani ya EFM iliyoko Kawe Beach Jijini Dar es Salaam. Katika kile kilichoelezwa kuwa ni sapraizi kwa mashabiki,jana EFM walimtambulisha msanii, Elizabeth Michael ‘Lulu’ asubuhi kama  mbadala wa Kitenge na kuibua gumzo.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad