Mahakama Yaamuru Tanzania Kuilipa IPTL Sh426 bilioni


Dar es Salaam. kutokana na mgogoro uliopo kati ya Tanesco na kampuni ya IPTL, mahakama ya migogoro ya kimataifa (ICSID) imeiamuru Serikali ya Tanzania kulipa Dola 185.4 milioni (zaidi ya Sh426 bilioni) kwa kukiuka mkataba.

Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) liliingia makubaliano ya kuzalisha umeme na IPTL (Independent Power Tanzania Limited) mwaka 1995 lakini mwaka 2013 kukawa na kutoelewana kati ya wahusika wa mkataba huo.



NAFASI ZA AJIRA ZILIZOTANGAZWA LEO BONYEZA HAPA

Katika makubaliano hayo, IPTL iliyokuwa inamilikiwa kwa ubia kati ya kampuni ya Mechmar ya Malaysia na VIP Engineering and Marketing ya Tanzania ilitakiwa kuzalisha megawati 100 kwenye mitambo yake iliyosimikwa Tegeta jijini Dar es Salaam na kuiuzia Tanesco.

Kutekeleza mkataba huo, IPTL ilikopa fedha kutoka kwa taasisi tofauti za fedha zikiwamo benki za nchini Malaysia kwa ahadi ya kurejesha kutokana na mapato itakayokuwa inayapata ikilipwa na Tanesco.

Mwananchi
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad