Mtibwa Sugar Wawekwa Njia Panda na Bodi ya Ligi

Uongozi wa klabu ya Mtibwa Sugar hadi sasa upo njia panda kufuatia kufungiwa kwa viwanja vyake vyote ilivyokuwa inachezea mechi za nyumbani kunako Ligi Kuu Bara.

Ikiwa ni wiki kadhaa tangu kufungiwa Uwanja wa Manungu, Mtibwa ilipangiwa kutumia uwanja wa Jamhuri ambao nao wiki hii umetangazwa kufungiwa na Bodi ya Ligi.

Saleh Jembe ilizungumza na Ofisa Habari wa Mtibwa, Thobias Kifaru, ambaye aliibuka na kusema kuwa hadi sasa wapo njia panda kuwa watatumia uwanja gani.

"Kiukweli hatujajua maana Manungu ilifungiwa na sasa Jamhuri nayo pia imefungiwa.

"Tunachoomba sisi TFF na Bodi ya Ligi waturuhusu tutumia huu wa Manungu sababu tunaingia kwenye gharama kubwa sana kupeleka timu Jamhuri, inakuwa kama tunaenda ugenini.

"Tunawaomba TFF watusaidie kwa hili hata kwa kipindi hiki tukiwa tunaelekea kujenga uwanja wetu wenyewe."
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad