Mume Amkata Masikio Mkewe kwa Kupoteza Simu


MKAZIwa Kijiji cha Mesaga Wilayani Serengeti Mara, aitwaye Magori anadaiwa kumkata masikio yote mawili Mke wake Mkami Mwitonyi mwenye umri wa miaka 22 kwa madai ya kupoteza simu yake.



Imeripotiwa kuwa, mwanamke huyo amelazwa katika Hospitali ya DDH wodi ya Wanawake tangu juzi Jumatano, Oktoba 23, 2019 kwa matibabu zaidi.

Akisimulia tukio hilo Kaka wa Mwanamke huyo Muhoni Mbusi amedai ulitokea ugomvi kati ya wanandoa hao kisha Magori akachukua kamba na kumning’iniza Mkewe juu ya dari na kumkata sikio la kwanza na la pili huku akimwambia sali sala yako ya mwisho nakuchinja.



Inadaiwa kuwa wakati anajiandaa kumchinja mwanamke huyo alipiga kelele kwa nguvu majirani wakawahi kutoa msaada.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara Juma Ndaki amethibitisha na kusema wanaendelea kumtafuta mtuhumiwa ili afikishwe kwenye vyombo vya sheria.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad