Nai apata kigugumizi kumuongelea Moni

 
Video Vixen na mjasiriamali Official Nai, ameonekana kupata kigugumizi kizito kumuongelea mpenzi wake Moni Centrozone baada ya kuwepo kwa taarifa za sintofahamu kuhusu kuachana kwao.

Nai ameonekana kusita kuzungumzia kinachoendelea kati yao, alipodakwa na kamera za EATV & EA Radio Digital, ikiwa ni baada ya kusambaa kwa video fupi inayomuonesha akimlalamikia wanaume kuhusu mahusiano yake.

"Sipo tayari na sitaki kuongelea kuhusu mahusiano yangu, viko nje ya uwezo wangu kuviongelea, maana naweza kuleta utofauti pengineyo kama clip ilitembea tayari ishatembea kama kuna vingine vya kuongea tutafanya muda mwingine", amesema Nai.

"Kila mahusiano yana mambo yake, mimi sitaki tu kuongelea kwa sababu inawezekana nikaonekana nimehukumu mahusiano yangu. Halafu unajua mahusiano hayajifichi na mapenzi hayana siri ila utatamani watu, vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kumjua mpenzi wako",  ameongeza.

Wiki iliyopita mrembo huyo alipost picha ya ua jeusi, katika mtandao wa instagram, ikionesha hali ya kuachana na mpenzi wake Moni Centrozone, kisha akaandika sasa hivi yupo single.


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad