Rais Magufuli atembelea Hifadhi ya Taifa ya Katavi


Rais Magufuli jana ametembelea Hifadhi ya Taifa ya Katavi na kisha kuzungumza na Maafisa na Askari Wanyamapori wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) ambapo amewapongeza kwa kazi nzuri ya kuhifadhi wanyamapori ikiwemo kukabiliana na ujangili hali iliyowezesha kuongezeka kwa idadi ya wanyama wakiwemo wale waliokuwa hatarini kutoweka lakini amewasihi wachache miongoni mwao ambao wanashirikiana na wahalifu waache tabia hiyo.

“Wapo wenzenu wachache wanaoshirikiana na majambazi, waache na wakipatikana wa namna hiyo, peleka mahakamani wafunguliwe kesi ya uhujumu uchumi," amesema Rais Magufuli.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia wanyama aina ya viboko katika hifadhi ya Taifa ya Katavi  mara baada ya kusimama wakati akielekea Mpanda.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad