Yanga yaangukia kwenye milioni baada ya kuzikosa bilioni za CAF


Unaambiwa kama Yanga wangefanikiwa kuiondoa Zesco United katika Ligi ya Mabingwa Afrika juzi Jumamosi, timu hiyo ingejinyakulia dola za Kimarekani 550,000 ambazo ni sawa zaidi ya bilioni 1.5 za Kitanzania.

Licha ya kuzikosa dola hizo, lakini kwa kuwa inaendelea na mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika, Yanga sasa inaweza kuambulia dola 275,000 ambazo ni zaidi shilingi za Kitanzania, milioni 774.
Yanga ilitupwa nje ya michuano hiyo kwa kipigo cha bao 2-1 juzi Jumamosi na kufanya jumla ya matokeo hayo pamoja na mechi ya raundi ya kwanza iwe ni mabao 3-2.

Yanga itatwaa dola 275 endapo kama itatinga hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad