Mahakama: Tundu Lissu Amepona Lakini Anahofia Usalama Wake Kurudi Nchini


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imeelezwa kuwa aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ameshapona ila anashindwa kurudi nchini kwa kile alichokidai ni kuhofia usalama wake.

Hayo yameelezwa leo Novemba 21,2019 na Mdhamini wa Lissu, Ibrahim Ahmed, alipokuwa akiieleza mahakama hiyo juu ya afya ya Mwanasheria huyo wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Ahmed ameieleza mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, wakati wa kesi ya uchochezi inayomkabili mshtakiwa huyo na wenzake watatu ilipoitwa.

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Kichwa Mmeboroga na Ni Potoshi.

    Sahihi ingekuwa.

    Mdhami wa Lissu Anena.na siyo Mahakama

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad