Mama Ajifungua Watoto Mapacha Watano


Binti mmoja mkazi wa Kata ya Mwakibeta Jijini Mbeya ajulikanaye kwa jina la Emelia Joram (21), amejifungua watoto watano katika Hospitali ya Rufani ya Mkoa wa Mbeya huku mmoja kati yao akiwa amekufa.

Binti huyo alijifungua Oktoba 31 mwaka huu kwa upasuaji ambapo watatu kati yao ni wa kike na mmoja pekee ndiye wa kiume na wawili wapo kwenye chumba cha joto kutokana na kuzaliwa wakiwa na uzito pungufu.

Kutokana na hali hiyo wadau mbalimbali wameombwa kumsaidia kumsaidia mama huyo kwenye malezi ya watoto hao ili wakuwe katika hali nzuri.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad