Rhino wa The Mafik asema kesi bado ipo polisi


Mmoja wa wasanii wanaounda kundi la The Mafik aitwaye Rhino King, amesema kesi iliyohusisha kifo cha msanii mwenzao anayeitwa Mbalamwezi, bado ipo polisi na wao bado hawana majibu sahihi ya kuzungumza.


Wasanii wa kundi la The Mafik, kutokea kushoto ni Rhino King katikati marehemu Mbalamwezi na kulia Hamadai.

Rhino King ameeleza hayo kwenye mahojianio ya EATV & EA Radio Digital, baada ya kuulizwa kuhusu chanzo kilichopelekea kifo cha mwenzao, ambacho hakijatolewa ufafanuzi rasmi hadi leo hii.

"Nimekuja hapa kutambulisha ngoma yangu mpya, sikuja hapa kuzungumzia suala la msiba, na kama kungekuwa na sababu ya mimi kuzungumzia suala hilo, nafikiri polisi ndiyo wanaripoti zaidi ya mambo ya msiba kwa sababu mimi ni kama wewe sijui chochote, nimempoteza ndugu yangu ukiniuliza hivyo nitakosa majibu" amesema Rhino King.

Ikumbukwe tu wakati taariza za kifo cha Mbalamwezi kundi hilo lilisema kwa sasa hawana majibu kamili ya taarifa kuhusu chanzo cha kifo chake.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad