Shabiki wa Diamond Amvamia ALI Kiba na Kumrudishia Pencil Yake Iliyopotea....VIDEO



Hili ni tukio lilitokea leo katika mkutano wa alikiba aliokuwa akiongea na waandishi wa habari,

Kama umekuwa ukifuatilia katika mitandao ya kijamii, kijana huyu ame- trend siku za hivi karibuni baada ya kukumbatiwa na diamondplatnuz siku ya tamasha la jama festival lililofanyika katika uwanja wa taifa, mara baada ya tukio hilo bwana mdogo huyu aliweza kukaa majuma kadhaa pasipo kuoga wala kubadili nguo&viatu vyake hata wakati wa kulala..
Basi bwana mdogo katika hali isiyokuwa ya yakawaida leo tena kajitokeza katika shughuli ya ali, nae Ali pasipo hiyana akamruhusu azungumze dukuduku lake la moyoni japo kuna baadhi ya watu walimzuia kijana huyu...bwanadogo huyu alianza kwa kusema nanukuu "me nishabiki wa diamondplatnuz na napenda sana amani, juzi nilibahatika kupita katika ukurasa wako wa insta na kukuta ukiwa umelaumu kuhusu kuibiwa pencil yako, sasa basi kwa kuwa napenda muwe na amani nimeamua kukuletea pencil yako ili kuwepo na amani baina yenu.." Mwisho wa kunukuu..

Bwana mdogo huyu aliemalizia kauli yake kwa kumpatia alieibiwa pencil yake, japo alirudishiwa pencil yake mara baada ya alikiba kumfafanulia maana kamili ya pencil aliyokuwa akimaanisha!!

VIDEO:

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad