Waziri Ndalichako azindua chuo kipya cha VETA Kagera


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amezindua chuo kipya cha VETA Ndolage kilichopo Kamachumu Wilaya ya Muleba mkoani Kagera kilichokamilishwa kwa Shilingi milioni 281.

Ujenzi wa Chuo hicho ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya kushirikiana na Jamii kufikisha Elimu ya Ufundi karibu na Wananchi pamoja na kujenga Vyuo vya VETA katika kila Wilaya nchini ifikapo mwaka 2020.


Wizara imetenga zaidi Bilioni 40 katika mwaka wa fedha 2019/20 kwa ajili ya ujenzi wa Vyuo vya VETA vya Wilaya 25 nchini.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad