Wema "Wamekubali Wembamba Wangu"


MKALI wa filamu za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’, amesema miezi kadhaa nyuma watu walikuwa wakimbeza kutokana na kukondeana, lakini sasa wameukubali wembamba wake.


Akichonga na Shusha Pumzi, Wema alisema, siku za nyuma alikuwa akikutana na maoni mengi kwenye ukurasa wake wa Instagram ambapo watu walikuwa wakimshauri kurudisha mwili wake wa zamani (unene), lakini sasa wanamwambia awaelekeze kitu alichotumia hadi akakonda kwani amependeza.



“Sasa hivi kila mtu anaukubali wembamba wangu na kuupenda hivyo nao wanaomba ushauri wawe kama mimi,” alisema Wema.

Stori: Imelda Mtema

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad