Faru Vicky atangazwa mrithi wa kiti cha Faru Fausta ‘Bibi wa kreta’



Kufuatia kifo cha aliyekuwa faru mwenye umri mkubwa zaidi duniani, Fausta, Mamlaka ya eneo la Ngorongoro (NCAA), imemtangaza faru Vicky kuwa faru mwenye umri mkubwa zaidi nchini.

Faru Vicky anakadiriwa kuwa na miaka 49 kwa sasa na hivyo kuwa faru pekee anayeweza kukalia kiti cha Fausta ambaye alikufa akiwa chini ya uangalizi maalumu ndani ya bonde la Ngorongoro akiwa na miaka zaidi ya 57, na kuacha rekodi ya kuwa faru mweusi mwenye umri mkubwa kuliko wote duniani.

Mwili wa Faru Fausta kuhifadhiwa kama kivutio cha utalii
Kamishna wa uhifadhi katika mamlaka ya Ngorongoro, Dkt. Freddy Manongi amesema kwakuwa faru Fausta alikuwa akiishi ndani ya jengo maalumu, mamlaka ya Ngorongoro inafikiria pia kumhamishia faru Vicky ndani ya nymba ya marehemu Fausta ili kumsaidia na yeye katika kipindi cha uzee.

Ikumbukwe kuwa faru wnakadiriwa kufikisha umri wa miaka 35 hadi 40 wakiwa porini na huishi zaidi ya hapo wakiwa chini ya uangalizi maalumu.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad