FIFA Yashusha Neema Tanzania


Shirikisho la soka nchini TFF limesema katika kukuza maendeleo ya soka la Tanzania, FIFA wapo kwenye mpango wa kujenga vituo vya michezo hapa nchini.

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia ameyasema hayo leo kwenye mkutano mkuu wa TFF unaofanyika jijini Dar es salaam, ambao umehudhuriwa na wadau mbalimbali wa mpira.

Rais huyo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) amesema kuwa FIFA wameahidi kujenga uwanja mmoja hapa nchini.

England kujipima kwa Italia kabla ya Euro 2020
“FIFA wameahidi kujenga uwanja mmoja hapa nchini na tumekubaliana kujenga vituo viwili vya Soka (Technical Centres) kwa maeneo ya Tanga na Kigamboni-Dar es Salaam, ujenzi ambao mchakato wake umeshaanza na mapema mwakani ujenzi utaanza,” amesema Karia.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad