Mbivu na Mbichi ya Hukumu ya JAMAL Malinzi Kujulikana Leo.....


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo December 5, 2019 inatarajia kutoa hukumu katika kesi inayomkabili aliyekuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na wenzake.

Hukumu hiyo inatarajia kutolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya upande wa mashitaka na utetezi kumaliza ushahidi wao.

Hukumu hiyo ilishagonga mwamba kutolewa takribani mara mbili kutokana na sababu tofauti ikiwemo ya Hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo kuhamishwa Kituo cha kazi, kesi hiyo ilikuwa na mashtaka 30 lakini ilipofikia katika uamuzi wa kama washtakiwa wana kesi ya kujibu ama laah! walipunguziwa mashtaka 10 na kubakiwa na mashitaka 20.

Washtakiwa wengine waliobakia katika kesi hiyo ni Mhasibu wa TFF, Nsiande Mwanga, Katibu wa shirikisho hilo, Selestine Mwesigwa na Karani wa TFF, Flora Rauya, wanakabiliwa na mashtaka mbalimbali yakiwamo ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na utakatishaji wa Dola za Marekani 173,335.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad