Mchuano Mkali TUZO za SoundyCity...Diamond Platnumz Kinara Kwenye Mapendekezo

Burna Boy, Diamond Platnumz, Davido, Wizkid, Ray Vanny watamba nominations tuzo za Sound City 2020 nchini Nigeria, Nandy awapa kifua wasanii wa kike Afrika mashariki

Burna Boy amepata nominations 6, huku Diamond Platnumz akipendekezwa katika categories 4 ambazo ni Msanii Bora wa Mwaka Afrika, collabo bora ya mwaka(Inama), msanii bora wa kiume Afrika, na digital artist wa mwaka -

Rayvanny amependekezwa vipengele 3 ambavyo ni Wimbo bora wa mwaka afrika(Tetema), chaguo bora la watazamaji Afrika, na msanii bora wa pop wa mwaka Afrika

Nandy amepata nominations vipengele viwili vya msanii bora wa kike Afrika pamoja na msanii bora wa pop afrika

S2Kizzy anawania tuzo ya producer bora wa mwaka afrika

Harmonize amependekezwa kipengele kimoja cha chaguo la wasikilizaji afrika, Marioo kutoka Tanzania anawania
Msanii bora chipukizi

Kwa upande wa Kenya Otile Brown anawania msanii bora wa pop Afrika Huku Kaligraph Jones akiiwakilisha Afrika mashariki katika kipengele cha msanii bora wa hip hop Afrika -

Tuzo hizo zitafanyika tarehe 11 January nchini Nigeria
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad