Mtoto Mdogo Afariki Kwa Kula Kitimoto



Watu wawili wa Familia moja (Baba na Mtoto) wanashikiliwa na Polisi Mkoani Rukwa kufuatia kuwauzia Wanakijiji nyama ya nguruwe ambae alikuwa mzoga na kusababisha Mtoto wa miaka miwili Mariam Peter kufariki Dunia huku Watu wengine 16 wakikimbizwa Zahanati katika Kijiji cha Utengule Wilayani Kalambo, Rukwa .

Familia ya Osward Simpungwe ilichinja nguruwe ambae alikufa mwenyewe bila kujua kilichomua na kuuza nyama ambayo iliwaletea madhara walaji.

Mtoto Mariam aliumwa tumbo baada ya kula nyama hiyo iliyonunuliwa na Baba yake na akafariki wakati akikimbizwa Zahanati.

“Matukio ya kulishwa mizoga yanajirudia mara kwa mara hapa, Serikali ituletee Wataalam wa kukagua nyama kabla ya kuliwa”– Mwanakijiji
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad