Rayvanny “Alikiba alikuwa wa kwanza kufungua milango nje alivyoshirikiana na R Kelly akafuata Diamond, huo ndio ukweli”



Msanii wa muziki wa Bongo Fleva anayetamba na kibao NAOGOPA akitokea lebal ya WCB Rayvanny amefunguka kinagaubaga kuhusu maneno yanayoendelea kuenea mitandaoni kuhusiana na Diamond kujaza uwanja kwenye Tamasha lililofanyika nchini Siera Leone na watu kuanza kubeza kile alichokifanya Diamond, mbali na hilo Rayvanny amewaonya wale wanaokatisha watu tamaa hasa kumtukana Diamond na kusema endapo Diamond akisema aache kufanya show nje nani atatuwakilisha?

Rayvanny ameongeza kuwa “Ukiangalia katika muziki wetu wa Bongo Fleva Alikiba alivyoshirikiana na akina R Kelly ndio alifungua milango ya wasanii wengine kufanya kolabo nje ya nchi akafuata Diamond Platnumz na huo ndio ukweli”
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad