Mbwana Samatta Apiga Bao, Huku Genk Ikichezea Kichapo


By Eliya Solomon
LICHA ya kutimuliwa kwa Felice Mazzu, KRC Genk anayoichezea nahodha wa timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Mbwana Samatta imeendelea kufanya vibaya katika Ligi Kuu Ubelgiji wakipoteza mchezo wanne mfululizo.

Genk wakiwa nyumbani wamekumbana na kipigo mabao 2-1 kutoka kwa Sint-Truiden jana Jumamosi katika mchezo wa Ligi Kuu Ubelgiji.

Katika mchezo huo, Genk ilikuwa ya kwanza kupata bao la kuongoza dakika ya tisa ya  mchezo kupitia kwa  Samatta likiwa ni goli lake la saba msimu huu katika  michezo 16 wa Ligi Kuu  Ubelgiji.

Sint-Truiden walisawazisha ndani ya dakika hizo 45 za kipindi cha kwanza. Kipigo hicho cha Genk inaendelea kuwaondoa taratibu katika mstari wa kutetea ubingwa wa Ligi Kuu nchini humo maarufu kama Jupiler Pro.

KRC Genk tangu wamtupishe virago vyake Felice Mazzu na nafasi yake akachukua Hannes Wolf, wameshindwa kuibuka na ushindi wa mchezo hata mmoja katika mshindano yote.

Walianza kupoteza kwa mabao 2-0, Novemba 10 dhidi ya Gent, Novemba 23 wakatoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Royal Excel Mouscron, Novemba 27 katika Ligi ya Mabingwa Ulaya wakafungwa na Salzburg kwa mabao 4-1 huku mchezo wao wa mwisho kucheza ukiwa dhidi ya Sint-Truiden.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad