Sudan: Polisi wahukumiwa kifo kwa kumtesa na kumuua mwalimu


Mwalimu Ahmad al-Khair, 36 alifariki wakati ameshikiliwa na Polisi baada ya kukamatwa wakati wa maandamano ya kumtoa Rais Omar al-Bashir madarakani.

Inaelezwa kuwa hii ni moja ya kuhumu za mwanzo kabisa kutolewa mara baada ya machafuko ya kuleta utawala wa demokrasia nchini Sudan. Hakimu anasema kuwa hukumu hizo za kifo ni sehemu ya kutoa funzo.

Baada ya hukumu Jaji aliwauliza kaka wa al-Khair kama anataka polisi hao wasamehewe lakini alikataa na kusema anataka wauwawe, huku Mwanasheria wa upande wa watetezi anasema kuwa atakata rufaa.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad