Wema Sepetu Humuambii Kitu Kwa Danzak, Aunt!


WEMA Isaac Sepetu ‘Madam’ kutoka kiwanda cha Bongo Muvi, amefunguka kuwa, kwa sasa watu anaowahusudu kupita maelezo kwenye maisha yake ni shosti wake, Aunt Ezekiel na msanii wa Bongo Fleva, Hamdani Zakwani ‘Danzak’.

Wema amesema, kwenye maisha suala la kuwa na marafiki ni muhimu na ameshakuwa na marafiki wengi, lakini kwa sasa amekita nanga kwa wawili hao.

“Hawa ndiyo furaha yangu, hawa ndiyo wafariji wangu kwa sasa, namshukuru Mungu kwa kunipa watu hawa,” alisema Wema bila kufafanua kwa undani uhusiano wake na Danzak.

Danzak aliwahi kukiri kwamba anampenda Wema na yupo tayari kumuoa hivyo kitendo cha wawili hao kuwa karibu, lolote linaweza kutokea.

Stori: Imelda Mtema

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad