Zitto Kabwe Asema kusherehekea Uhuru ni Kuhalalisha Ukandamizaji


Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amesema  kusherehekea Uhuru na wanaokandiza Uhuru ni kuhalalisha ukandamizaji.

Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini aliandika ujumbe huo kupitia ukurasa wake wa Twitter kuwa kusherehekea Uhuru na wanaokandamiza Uhuru , Uhuru wa mawazo, Uhuru wa kufanya siasa na kuchagua viongozi.

“Rejea uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba 2019, Uhuru wa habari (#Azory # Kabendera # Mwanahalisi), Uhuru wa kuishi (#BenSaanane # Lissu  ni kuhalalisha ukandamizaji,” aliandika Zitto.

Kusherehea Uhuru na wanaokandamiza Uhuru – Uhuru wa Mawazo; Uhuru wa kufanya Siasa na kuchagua Viongozi ( rejea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 2019 ); Uhuru wa Habari ( #Azory #Kabendera #Mwanahalisi ); Uhuru wa kuishi ( #BenSaanane #Lissu ) ni kuhalalisha ukandamizaji.

— Zitto Kabwe Ruyagwa (@zittokabwe) December 8, 2019

Jana Chama cha Demokarasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza kushiriki maadhimisho ya kumbukumbu ya Uhuru wa Tanganyika ambayo kitaifa yanafanyika mkoani Mwanza.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad