Kenya yatoa Tahadhati Kuhusu Virusi vya Corona





Wizara ya afya nchini Kenya imeimarisha uangalizi katika bandari zake zote za kuingia na kufanya na kupima abiria kuona kama wana virusi vya corona, ambavyo mpaka sasa watu takribani 400 wana maambukizi na watu 9 wamepoteza maisha nchini China.

Kenya imekuwa ikipokea wageni wengi kutoka China.

Kenya ni moja kati ya nchi iliyo hatarini kukumbwa na virusi vya Corona kutokana na mahusiano ya kibiashara na China. Kila wiki, shirika la ndege la Kenya hupeleka ndege zake mbili kati ya jiji la Nairobi na Guangzhou.

Mamlaka za China zimewataka watu kutosafiri ndani na nje ya mji wa Wuhan, mji virusi hivi vilipoanzia kisha kusambaa katika majimbo kadhaa ya China, pia nchini Marekani, Thailand na Korea Kusini.

WHO inatazama kama mlipuko huu unaweza kuwekwa kwenye kundi la dharura ya kiafya kimataifa.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad