Mwanamuziki Drake Aanika Chanzo bifu na Chris Brown



RAPA Aubrey Graham maarufu kwa jina la Drake, amefunguka kwa mara ya kwanza chanzo cha mgogoro wake dhidi ya mkali wa muziki wa RnB nchini Marekani, Chris Brown.

Drake amesema wawili hao waliingia kwenye mgogoro kwasababu ya Rihanna, lakini anashukuru kila kitu kwa sasa kipo sawa na wamefanikiwa kufanya muziki wa pamoja.

“Chris alikuwa kwenye uhusiano na Rihanna kwa kipindi kirefu hadi wanakuja kuachana mwaka 2009, baada ya kuachana nikawa rafiki wa karibu na Rihanna jambo ambalo halikuwa sawa kwa Chris, lakini hakukuwa na kitu chochote kibaya na ndio maana kwa sasa sina tofauti na Chris.

“Ukweli ni kwamba wanawake wamekuwa sababu kubwa ya migogoro, nadhani kwa sasa Rihanna atakuwa anaumia akiwa anaona au kusikia kuwa nipo karibu na Chris,” alisema msanii huyo.


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad