Tanasha Donna Avunja UKIMYA Kuhusiana na Madai ya Diamond Kuwa na Mpenzi Mwingine



Mpenzi Mkenya wa msanii Diamond Platinumz, Tanasha Donna hatimaye amevunja kimya chake baada ya kuibuka kwa maneno kuwa mwanamuziki huyo ana uhusiano wa pembeni.

Diamond anadaiwa kuwa katika uhusiano mwingine na mrembo wa Tanzania yapata miezi sita tu baada ya kumkaribisha mwanawe wa kiume Naseeb Junior.

Mama huyo wa mtoto mmoja kupitia ukurasa wake wa Instagram, aliwaomba watu kukoma kueneza habari ambazo macho yao hayajashuhudia kwa kutumia mdomo.

Ni bayana kuwa mrembo huyo alikuwa anajibu madai kuwa mpenziwe ana uhusiano na mwanadada kwa jina Rose.

Katika hali ya kuzima fununu kuhusu uhusiano wake, mtangazaji huyo wa radio ya NRG alisema mapenzi yake na Diamond hayawezi kuvunjika.

Donna alichapisha picha yake na Diamond katika hali ya mahaba na kuonyesha kuwa hawawezi kutengana hivi karibuni.


Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad