Trump: Iran Wakithubutu Kulipa Kisasi Tutashambulia Maeneo Yao 52 Ndani ya Dakika Chache



Rais Donald Trump wa Marekani ameonya kuwa nchi yake itayashambulia haraka na vikali maeneo 52 ya Iran iwapo Jamhuri hiyo ya Kiislam itafanya mashambulizi dhidi ya raia wa Marekani na mali zake kulipiza kisasi kwa mauaji ya Jenerali Qassem Soleimani.

Katika ujumbe wa kitisho kupitia ukurasa wa Twitter, Trump amesema maeneo yatakayolengwa ni yale yaliyo muhimu kwa Iran na utamaduni wake na kuonya Marekani haiko tayari kuendelea kutishwa na Iran.

Ujumbe huo wa Trump unafutia onyo la makundi ya wanamgambo yanayoiunga mkono Iran la kuvishambulia vituo vya Marakani nchini Iraq kutokana na mauaji ya kamanda huyo muhimu wa jeshi la Iran.

Isikupite Hii: Ajira Mpya Zilizotangazwa Wiki Hii ...Soma Hapa

Katika ishara za mwanzo za uwezekano wa kulipa kisasi, makombora mawili yalilipiga eneo lililo karibu na ubalozi wa Marekani mjini Baghdad siku ya Jumamosi.

Makombora mengine mawili yaliishambulia kambi ya kijeshi ambayo inahifadhi wanajeshi wa Marekani lakini hakuna athari kubwa zilizoripotiwa.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad