Amber Rutty Amwaga Machozi "Wanatamani Nife"


Msanii na Video Vixen hapa nchini Amber Rutty,  amefunguka mazito hadi kufikia hatua ya kumwaga machozi baada ya kusema kuna baadhi ya watu wanatamani asiwepo duniani na wengine wanamchukulia kama mkosefu mkubwa katika jamii.


Amber Rutty ameeleza hayo mbele ya waandishi wa habari leo Februari 19,2020, wakati anaomba msamaha na kutaka watu wampokee katika jamii pamoja na kueleza historia ya maisha yake.

"Mimi nimekuwa mtu wa kupata matatizo kila siku kwenye maisha yangu yote, kuanzia utotoni hadi hapa nilipofikia, ninachoweza kusema kwa ndugu,jamaa, na Watanzania wote wanisamehe maana sijaona kosa langu lilipo, japo watu wananichukia na kuniona binadamu mkosefu kuliko mtu yeyote hapa Duniani" ameeleza Amber Rutty.
HIZI HABARI ZA HIVI ZINAPATIKANA UDAKU SPECIAL >>BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL

Aidha msanii huyo ameongeza kusema
"Najikuta mnyonge kwa binadamu wenzangu ambao wanajiona wamekamilika, kuna baadhi ya watu wanajua umuhimu wangu kuna wengine wananiona sio binadamu kamili natakiwa nife na katika Dunia hii nisionekane tena"

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad