Esther Passaris Amtuliza Jamaa Aliyeachwa na Mpenzi wake Siku ya Wapendanao


Mwakilishi wa kina mama kaunti ya Nairobi Esther Passaris amempa pole jamaa ambaye alibaki na kilio baada ya mpenzi wake kumuacha.

Passaris amemtaka kuvumilia kuachwa na aendelee na maisha licha ya uchungu ambao anapitia baada ya jamaa mwingine kuvuka na mpenzi huyo wake.

Esther Passaris amemtuliza jamaa aliyeachwa na mpenzi wake siku ya wapendanao. Picha Esther 
Moody Bick alisema alikuwa ameumia pakubwa moyoni baada ya binti aliyekuwa amemtunza kwa miaka mitatu kumhepa siku ya valentines.

Kulingana na Bick, binti huyo alikataa waonane na badala yake akamuendea mwanaume mwingine aliyesema anampenda.

"Niko katika hali ya kuruka akili baada ya mpenzi wangu wa miaka mitatu kunitumia ujumbe kuwa hataweza kujibu simu zangu kwa sababu anajivinjari na mpenziwe," alisema.

Passaris ambaye alikuwa amewataka wanamtandao kumsimulia jinsi ambavyo siku yao ya wapendanao imekuwa aliguzwa na hali ya Bick.

"Hivyo ndivyo maisha yalivyo. Vumilia hali na uendelee na maisha. Kama unampenda, elewa ni kwa nini alikuwacha na urekebishe. Kila la heri," alisema Passaris.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad