Freeman Mbowe Akamatwa na Polisi Akidaiwa Kutoa Maneno ya Uchochezi



CHADEMA imesema Mwenyekiti wake na Mbunge wa Jimbo la Hai, Freeman Mbowe amekamatwa na Polisi baada ya kumaliza mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Masama Kati, Kijiji cha Lemira Kati viwanja vya Nkoromu

Inadaiwa kuwa Polisi wamevamia msafara alipomaliza mkutano, wakaingia ndani ya gari lake kwa nguvu na kuamuru liekelee kituoni Bomang'ombe

Aidha, kimedai kuwa katika mahojiano yanayoendelea kwa takriban saa 3, Polisi wanadai Mbowe amezungumzia masuala ya Tume Huru ya Uchaguzi, hali ya demokrasia nchini, badala ya maendeleo ya jimbo

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Salum Hamdun amesema Mbowe amekamatwa na Polisi baada ya kutoa maneno ya uchochezi yanayoashiria uchochezi, kuamsha hisia na chuki dhidi ya Serikali na Polisi
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad