Halima Mdee Agoma Kumpa Mkono aliyekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk.Vincent Mashinji



Baada ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk.Vincent Mashinji kuhamia CCM, leo Februari 24, amekutana na viongozi wa CHADEMA katika Mahakama ya Hakimu Mkazi kwa ajili ya kesi yao ya uchochezi inayowakabili mahakamani hapo.

Mashinji alifika mahakamani hapo kisha akaanza kusalimiana na viongozi mbalimbali wa CHADEMA ambao wapo katika kesi moja.

Miongoni mwa aliosalimiana nao ni Mbunge wa Bunda, Ester Bulaya, Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa, Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko na Salum Mwalimu.

Hata hivyo, katika hali isiyo ya kawaida Mbunge wa Kawe, Halima Mdee alikataa kupeana mkono na Mashinji.

Pia Dr.Mashinji alionana na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe wakiwa ndani ya chumba cha Mahakama licha ya kuwa hawakupeana mikono.

Kesi hiyo imeitishwa leo mahakamani hapo kwa ajili ya kufanya majumuisho ya mwisho kabla ya kutolewa hukumu.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad