Jacqueline Mengi azuiwa kuingia kwenye kaburi la mumewe afunguka mazito anayofanyiwa



Mwadadada Jacqueline Mengi ambaye alikuwa mke wa Mke wa Mkurugenzi wa Makampuni ya IPP Reginald Mengi ambaye kwa sasa ni marehemu ameeleza magumu anayopitia hivi sasa.

Jacqueline ambaye amebaatika kupata watoto wawili ambao ni mapacha wa mzee Mengi ameamua kuvunja ukimya na kufunguka mitihani anayopitia kwa sasa ikiwemo kukatazwa kufika kwenye kaburi la marehemu mume wake.

Kupitia akaunti yake ya twitter amepost picha akiwa na mumewe pamoja na watoto wake na kuandika hivi;

"Nimenyamaza kwa mengi sana tu.Mmefikia hatua ya kunizuia mimi na wanangu kuingia kwenye kaburi la mume wangu,tunafukuzwa eti mpaka tuombe ruhusa ya kuingia kwenye kaburi la mume na Baba wa watoto wangu!.Nimechoka,sitakubali kuendelea kuona wanangu wakisononeka na sitakaa kimya".


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad