Jasusi wa CIA Ahukumiwa Kunyongwa Nchini Iran


Msemaji wa Idara ya Mahakama nchini Iran Bw. Gholam Hossein Esmaili, amesema Mahakama Kuu ya nchi hiyo imemhukumu kifo raia mmoja wa Iran ambaye ni jasusi wa Shirika la Upelelezi la Marekani, CIA.

Shirika la habari la Iran Fars limemnukuu Bw. Esmaili akisema kuwa, Amir Rahimpour, ambaye alikuwa mpelelezi wa CIA, alipewa kiasi kikubwa cha pesa ili kutoa baadhi ya taarifa kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran kwa idara ya ujasusi ya Marekani.

Ameongeza kuwa watu wengine wawili wamehukumiwa kifungo cha miaka 10 kila mmoja gerezani kwa tuhuma za kufanya upelelezi kwa ajili ya Marekani.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad