Miili ya watu 20 waliofariki kwenye kongamano la Mtume na Nabii Mwamposa Kuagwa Kesho


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira, amesema miili ya watu 20 waliofariki kwenye kongamano la Mtume na Nabii Mwamposa, itaagwa kesho Februari 3, 2020, kwenye viwanja vya Majengo mjini Moshi.  Amesema hadi sasa tayari miili 16 imeshatambuliwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini ,IGP Simon Sirro amewataka Watanzania kuwa  makini kwani kinyume na hapo itakuwa shida sana na kuongeza iko haja kamati za ulinzi na usalama za wilaya na mkoa kuanza kuyafuatilia makanisa yote nchini na hasa makanisa madogo madogo ambayo sasa yamekuwepo kila mahali.

"Sio kila padri, mchungaji basi anataka kuwachunga kondoo wake waende kuuona ufalme wa Mungu, wengine wanahangaika na utafutaji tu wa maisha.Sio kwamba nahukumu lakini kuna mambo ya kujifunza,"amesema

Kuhusu Polisi iwapo walikuwepo kwenye kongamano hilo la Mwamposa, IGP Sirro amesema ameshatoa maagizo kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimajaro kufuatilia na iwapo walikuwepo polisi lazima waulizwe imekuaje hadi watu wakapoteza maisha na wao wakiwepo, kwani sheria lazima ichukue mkondo wake.
Tags

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Poleni Wafiwa.
    Naomba Serikali na Viongozi wa makanisa yote nchini na wana taaluma
    na baraza la Lugha yetu fasihi ya Kiswahili Uhalali wa kutumia s
    Siafa ya Kujiita NABII au MTUME.!!

    Na sifa ambatanishi zilizotukuka.

    TUJUE NA KUPIGA MARUFUKU UTAPELI
    NA UTUMIAJI HARAMU KUJIPATIA KIPATO
    WASICHO STAHILI.

    NABII..??? MTUME..???
    JAMANI MNPOTOSHA LUGHA YETU.
    HAMUITENDEI HAKI.

    ReplyDelete
  2. Poleni Wafiwa.
    Naomba Serikali na Viongozi wa makanisa yote nchini na wana taaluma
    na baraza la Lugha yetu fasihi ya Kiswahili Uhalali wa kutumia s
    Siafa ya Kujiita NABII au MTUME.!!

    Na sifa ambatanishi zilizotukuka.

    TUJUE NA KUPIGA MARUFUKU UTAPELI
    NA UTUMIAJI HARAMU KUJIPATIA KIPATO
    WASICHO STAHILI.

    NABII..??? MTUME..???
    JAMANI MNPOTOSHA LUGHA YETU.
    HAMUITENDEI HAKI.

    ReplyDelete
  3. Binafsi i feel sorry ila ujinga wao ndio umewapeleka kwa nabii fake. Wacha wajifie, ndio nchi pia itajisafisha maana wajinga wamekuwa wengi.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad