Shirika la Reli Latangaza Kusitisha Huduma RELI ya Kati...



Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania – TRC Ndugu Masanja Kungu Kadogosa kupitia JamiiForums imeeleza huduma za usafiri wa treni za abiria na mizigo kwa reli ya kati zimesitishwa

Hii ni kutokana na uharibifu wa njia ya reli uliosababishwa na mafuriko maeneo ya Kilosa, Igandu, Dodoma na Makutupora

Imefafanuliwa kuwa mvua zinazoendelea kunyesha Ukanda wa Kati zimeleta uharibifu mkubwa katika njia ya reli hasa maeneo ya Kilosa (Morogoro), Gulwe (Mpwapwa), Igandu, Zuzu na Makutupora (Singida)

Maeneo 26 yameathirika kati ya hayo 10 yako katika hali mbaya ambapo tuta la reli na baadhi ya Makalavati yamesombwa na mafuriko

TRC imeanza kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kujaza vifusi katika maeneo yaliyoathirika kuanzia Kilosa hadi Igandu ili kurudisha mawasiliano katika maeneo hayo

NB: Picha si halisi kwa habari hii
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad