Wanafunzi 14 wafariki kwa kukanyagana Kenya



Wanafunzi 14 wamefariki dunia huku wengine 39 wakijeruhiwa katika Shule ya Msingi Kakamega nchini Kenya kutokana na kukanyagwa na wenzao na kuanguka wakati wakikimbia.

Ajali hiyo imetokea Jumatatu Februari 3 majira ya saa 11 joni wakati watoto hao wakitoka madarasani kurejea makwao, ambapo tayari wanafunzi 20 waliojeruhiwa wameruhusiwa kutoka hospitali.

“Kumpoteza mtoto ni tukio linalouma sana. Natoa salamu za pole kwa wazazi wote waliofiwa na watoto wao,” Waziri wa Elimu, George Magoha amesema.

Kamanda wa Polisi wa Kakamega, David Kabena amesema chanzo cha tukio hilo hakijafahamika lakini amebainisha kuwa tayari uchunguzi umeanza.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad