Web

Abiria Watakiwa Kuosha Mikono na Vyombo na Vyombo vya Usafiri Kupuliziwa Dawa




Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini Tanzania (LATRA) imeyataka mabasi ya usafirishaji abiria maarufu 'daladala' katika mikoa yote Nchini kubeba watu kulingana na idadi ya siti zilizopo

Imetoa maagizo hayo baada ya kukutana na wadau wa usafiri na usafirishaji, kutafakari na kuweka mikakati ya kukabiliana na kasi ya kusambaa kwa #COVID19

Pia, magari hayo yanapaswa kunyunyiziwa dawa kila mwisho wa safari na kuwa na dawa ya kuua wadudu mikononi (hand sanitizer) ili kila abiria apake kabla ya kuingia

Mabasi yaendayo haraka (BRT) yametakiwa kubeba idadi ya abiria kulingana na idadi iliyoainishwa kwenye leseni zao na magari ya mizigo hayaruhusiwi kubeba abiria

Shirika la Reli Tanzania (TRC) wametakiwa kuhakikisha treni zinapuliziwa dawa za kuua virusi kila mwisho wa safari na abiria wanapoingia Kituoni kunawa kwa sabuni na maji tiririka

Aidha, Waendesha taksi, pikipiki za magurudumu mawili na matatu wametakiwa kuhakikisha abiria wanapaka dawa ya kuua virusi mikononi (hand sanitizer) kabla ya kupanda kwenye chombo husika

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad