Kenya yasimamisha safari za ndege kutoka Kaskazini mwa Italia



Serikali ya Kenya imesimamisha safari za ndege kutoka Kaskazini mwa Italia kutokana na mlipuko wa nimonia ya COVID-19 nchini humo.

Mwenyekiti wa Kamati ya kitaifa ya mwitikio wa dharura dhidi ya COVID-19 Bw. Mutahi Kagwe, amesema safari za ndege kutoka Kaskazini mwa Italia, hasa miji ya Verona na Milan, kwenda mkoa wa pwani nchini Kenya zimesimamishwa kuanzia tarehe 3 mwezi Machi.

Bw. Kagwe ambaye pia ni waziri wa afya wa Kenya amesema, Kenya itaendelea kufuatilia hali ya nchini Italia na kurekebisha sera yake kulingana na maendeleo ya hali.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad