Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi, Christopher Ngubiagai amekemea kitendo hicho na kuahidi kuwachulia hatua kali wote waliohusika
Baadhi ya wananchi wa Wilayani humo wamewazomea watalii wa kizungu waliotembelea Wilaya hiyo kuangalia mambo mbalimbali ya kihistoria
Pia, Ngubiagai ameagiza Taasisi zote binafsi na za Umma Wilayani humo kutengeneza sehemu ya kunawia mikono watu mbalimbali pindi waingiapo katikaofisi zao
Mpaka sasa Mataifa 180 yameathirika kutokana na virusi hivyo huku watu 246,972 wakiathirika, watu 10,050 wakipoteza maisha na 88,486 wakipona virusi hiyo